October 7, 2024

Bajeti Kuu Tanzania yapaa miaka minne mfululizo

Bajeti hiyo imekuwa ikiongezeka kila mwaka tangu mwaka wa fedha wa 2016/17.

Dar es Salaam. Wakati Watanzania wakisubiri kwa hamu kusikia mapato na matumizi ya Serikali kwa mwaka 2020/21, bajeti hiyo imekuwa ikiongezeka kila mwaka tangu mwaka wa fedha wa 2016/17. 

Pia ni bajeti mwisho katika awamu ya kwanza ya miaka mitano ya uongozi wa Rais John Mgufuli tangu alipoingia madarakani mwishoni mwaka 2015.