October 7, 2024

Majaliwa ashikilia hatma ya DED Lindi

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Shaibu Ndemanga ampelekee taarifa ya utendaji kazi wa Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Waryoba Gunza baada ya kushindwa kutoa maelezo kuhusu utekelezaji wa mradi wa maji kata ya Rutamba.